Al Ahly wamelinda nafasi yao ya kwanza kundi D baada ya ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Yanga katika mchezo wa kuhitimisha hatua ya makundi uliopigwa uwanja wa Kimataifa wa Cairo
Bao pekee la Al Ahly lilipatikana mwanzoni mwa kipindi cha pili kupitia kwa Hussein El Shahat
Ulikuwa mchezo mzuri kwa kila upande, Yanga wakicheza kwa kuwaheshimu Al Ahly zaidi
Yanga ilitengeneza nafasi bora zaidi za kufunga kwenye kipindi cha kwanza lakini Pacome Zouzoua na Joseph Guede hawakutumia vyema nafasi
Wananchi sasa wanasubiri droo ya hatua ya robo fainali ambapo mchezo wa kwanza wataanzia nyumbani na kumalizia ugenini



