Al Ahly yaichapa Yanga 1-0

Joel JJ By Joel JJ β€’ 1st March 2024


Al Ahly yaichapa Yanga 1-0

Al Ahly wamelinda nafasi yao ya kwanza kundi D baada ya ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Yanga katika mchezo wa kuhitimisha hatua ya makundi uliopigwa uwanja wa Kimataifa wa Cairo

Bao pekee la Al Ahly lilipatikana mwanzoni mwa kipindi cha pili kupitia kwa Hussein El Shahat

Ulikuwa mchezo mzuri kwa kila upande, Yanga wakicheza kwa kuwaheshimu Al Ahly zaidi

Yanga ilitengeneza nafasi bora zaidi za kufunga kwenye kipindi cha kwanza lakini Pacome Zouzoua na Joseph Guede hawakutumia vyema nafasi

Wananchi sasa wanasubiri droo ya hatua ya robo fainali ambapo mchezo wa kwanza wataanzia nyumbani na kumalizia ugenini


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.