Ukata waiweka matatani Singida FG

Joel JJ By Joel JJ β€’ 5th March 2024


Ukata waiweka matatani Singida FG

Jana klabu ya Singida FG ilithibitisha kuachana na kiungo Bruno Gomez, raia wa Brazil

Gomez alifikia makubaliano ya pande mbili kuachana na Singida FG kwa kile kinachoelezwa timu hiyo kushindwa kumlipa stahiki zake kwa wakati

Huu unaweza kuwa mwendelezo wa Singida FG kusambaratika ikiwapoteza nyota wake muhimu waliojiunga na timu nyingine

katika dirisha dogo la usajili nyota sita wa kigeni waliachana na timu hiyo na kutimkia Ihefu Fc ambayo ilipata mmiliki mpya baada ya kuuzwa

Ihefu Fc imehamishia makazi yake Singida ikitumia uwanja wa LITI wakati Singida ikihamishia makazi yake Mwanza ikitumia uwanja wa CCM Kirumba

Mpaka sasa Singida FG wamecheza mechi nane mfululizo za ligi kuu pasipo kupata ushindi


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.