Jana klabu ya Singida FG ilithibitisha kuachana na kiungo Bruno Gomez, raia wa Brazil
Gomez alifikia makubaliano ya pande mbili kuachana na Singida FG kwa kile kinachoelezwa timu hiyo kushindwa kumlipa stahiki zake kwa wakati
Huu unaweza kuwa mwendelezo wa Singida FG kusambaratika ikiwapoteza nyota wake muhimu waliojiunga na timu nyingine
katika dirisha dogo la usajili nyota sita wa kigeni waliachana na timu hiyo na kutimkia Ihefu Fc ambayo ilipata mmiliki mpya baada ya kuuzwa
Ihefu Fc imehamishia makazi yake Singida ikitumia uwanja wa LITI wakati Singida ikihamishia makazi yake Mwanza ikitumia uwanja wa CCM Kirumba
Mpaka sasa Singida FG wamecheza mechi nane mfululizo za ligi kuu pasipo kupata ushindi



