Manara ataka Dube achangiwe

Joel JJ By Joel JJ β€’ 5th March 2024


Manara ataka Dube achangiwe

Msemaji wa zamani wa Yanga Haji Manara amewataka wadau wa soka kumchangia mshambuliaji Prince Dube ambaye ameandika barua ya kuomba kuvunja mkataba wake na matajiri wa Chamazi, Azam Fc

Manara amebainisha kuwa kama alivyochangiwa Feisal Salum katika jitihada zake za kuondoka Yanga basi Wananchi nao wamchangie Dube

"Wananchi naomba na sisi tumchangie Dube Prince kama alivyochangiwa Fei," aliandika Manara katika ukurasa wake wa mtandao wa kijamii

Jana klabu ya Azam Fc ilithibitisha kupokea barua ya Dube aliyeomba kuvunja mkataba wake ili akatafute changamoto sehemu nyingine

Afisa Habari wa Azam Fc Thabit Zacharia 'Zakazakazi' alisema mkataba wa Dube na Azam Fc unamalizika mwaka 2026 lakini wako tayari kumuachia mchezaji huyo iwapo atafuata taratibu za kuvunja mkataba huo

Zakazakazi alisema gharama ya kuvunja mkataba uliobaki ni dola laki tatu (zaidi ya Mil 800) huku akitangaza watapokea ofa ya timu yoyote inayomtaka mchezaji huyo raia wa Zimbabwe

Hata hivyo baadhi ya wadau wa soka nchini wamewataka Azam Fc kuwa waungwana kwa Dube ambaye amewatumikia kwa moyo mmoja tangu alipojiunga nao mwaka 2020


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.