Transfer - International

Tetesi za soka Ulaya, Jumanne March 05 2024

Joel JJ By Joel JJ
β€’
5 Mar 2024
Tetesi za soka Ulaya, Jumanne March 05 2024

Manchester United na Paris St-Germain wanaibuka kuwa mstari wa mbele kumsajili mshambuliaji wa Napoli na Nigeria Victor Osimhen, 25, msimu huu. (Independent)

Newcastle United wanakaribia kukubaliana kandarasi mpya na Joelinton, huku kiungo huyo wa kati wa Brazil mwenye umri wa miaka 27 akiwa amebakiza kidogo zaidi ya mwaka mmoja katika mkataba wake wa sasa. (Telegraph )

Tottenham Hotspur wametuma maskauti kwenda kumwangalia mchezaji wa Sporting Lisbon Morten Hjulmand, kiungo wa kati wa Denmark mwenye umri wa miaka 24 (Record, via Sun)

Chelsea imewataja wachezaji wa Brighton Roberto de Zerbi na Ruben Amorim wa Sporting kama wanaoweza kuchukua nafasi za Mauricio Pochettino. (Guardian)

Wachezaji kadhaa wa Manchester United wanaamini kuwa meneja wa Uholanzi Erik ten Hag atabadilishwa mwishoni mwa msimu huu na wamiliki wenza wapya Ineos. (Mail)

Kocha wa Tottenham Ange Postecoglou atakataa ofa zozote za kuondoka msimu huu wa joto, ikiwa ni pamoja na kutoka kwa Liverpool. (Football Insider)

Manchester United inakusudia kumuuza winga wa Uingereza Jadon Sancho msimu huu wa joto kufuatia kipindi cha mkopo cha mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 23 na Borussia Dortmund, bila kujali kama Erik ten Hag bado ni meneja wa United. (Football Insider)

Newcastle wanapanga kumpeleka winga wa Gambia Yankuba Minteh kwa mkopo kwa msimu wa pili mfululizo. Minteh, ambaye Magpies walimsajili kutoka klabu ya Denmark Odense Boldklub kwa £6m msimu uliopita, amekuwa katika klabu ya Feyenoord ya Uholanzi msimu huu. (i)

Liverpool huenda ikalazimika kuilipa Bayer Leverkusen ada iliyovunja rekodi ya dunia ya pauni milioni 21 ili kumrejesha Xabi Alonso Anfield msimu huu wa joto ikiwa ni mara mbili ya ile waliyolipa kumsajili Mhispania huyo kama mchezaji. (Mirror)

Real Madrid wako tayari kuongeza ofa yao kwa mlinzi wa kushoto wa Bayern Munich Alphonso Davies, 23, hadi £43m. (Cadena Ser, kupitia Mundo Deportivo)

Kocha wa Burnley Vincent Kompany anaendelea kuungwa mkono na uongozi wa klabu hiyo, licha ya matumaini yao ya kunusurika katika Ligi ya Primea kutokana na kushindwa tena dhidi ya Bournemouth Jumapili. (Athletic)

Mustakabali wa kifedha wa Everton utawekwa shakani mwishoni mwa mwezi huu ikiwa pendekezo la kuchukua 777 Capital bado halijatatuliwa. (Telegraph )

Chelsea ilituma maskauti kumtazama mlinzi Mwingereza Archie Brown, 21, ambaye anachezea Gent ya Ubelgiji, wikendi. Kinda huyo wa zamani wa Derby County pia anatazamwa na Leeds United na West Ham United. (HITC)

BBC

More Stories

Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
45m ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
1h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
1h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
2h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
3h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
4h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
4h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
18h ago
READ MORE β†’