Mshambuliaji Prince Dube ametangaza kuachana na klabu ya Azam Fc baada ya kuitumikia kwa misimu minne
Dube amewaaga Azam Fc kupitia ukurasa wake wa mtandao wa Instagram
Wakati Dube akiaga, uongozi wa Azam Fc umesisitiza kuwa mchezaji huyo bado ni mali yao mpaka pale atakapotekeleza taratibu za kuvunja mkataba wake
Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano klabu ya Azam Fc Thabit Zacharia 'Zakazakazi' amesema wamemwambia Dube asome mkataba wake vyema na ahakikishe umeuelewa kisha afuate maelekezo yanayomtaka nini afanye ili avunje mkataba huo




