Dube aaga, Azam Fc wagoma

Joel JJ By Joel JJ β€’ 7th March 2024


Dube aaga, Azam Fc wagoma

Mshambuliaji Prince Dube ametangaza kuachana na klabu ya Azam Fc baada ya kuitumikia kwa misimu minne

Dube amewaaga Azam Fc kupitia ukurasa wake wa mtandao wa Instagram

Wakati Dube akiaga, uongozi wa Azam Fc umesisitiza kuwa mchezaji huyo bado ni mali yao mpaka pale atakapotekeleza taratibu za kuvunja mkataba wake

Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano klabu ya Azam Fc Thabit Zacharia 'Zakazakazi' amesema wamemwambia Dube asome mkataba wake vyema na ahakikishe umeuelewa kisha afuate maelekezo yanayomtaka nini afanye ili avunje mkataba huo


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.