Liverpool wameungana na Arsenal na Manchester United kuonyesha nia ya kumnunua winga wa Borussia Dortmund na Uholanzi Donyell Malen, 25. (Bild - in German)
Mkufunzi wa West Ham David Moyes anapanga ofa mpya ya kumnunua kiungo wa kati wa Manchester United Harry Maguire, 31, msimu wa joto. Sun)
Mshambulizi wa England Marcus Rashford, 26, anatazamiwa kugoma kuhamia Paris St-Germain na kusalia Manchester United. (Sun)
Atletico Madrid wameuliza kuhusu uhamisho wa mshambuliaji wa Uingereza Mason Greenwood, 22, lakini Manchester United wameweka dau la pauni milioni 50. (Football Transfers)
Wachezaji wenzake Greenwood katika klabu ya Manchester United wamemtaka kurudi katika klabu hiyo baada ya muda wake wa mkopo Getafe. Sun) Mchezaji anayelengwa na Chelsea Leny Yoro anataka kujiunga na Real Madrid, ingawa Lille wanaomba euro 100m (£85.6m) kwa mlinzi huyo wa Ufaransa, 18. (Marca - in Spanish)
Newcastle United italazimika kumuuza mmoja wa wachezaji wao muhimu msimu huu wa joto katika juhudi za kusawazisha vitabu vyao. (Football Insider)
Christian Eriksen ataondoka Manchester United mwishoni mwa msimu huu ikiwa ofa inayofaa itapatikana kwa kiungo huyo wa kati wa Denmark mwenye umri wa miaka 32. (Footbal Transfers) Brighton wanamfuatilia winga wa Arsenal Muingereza Reiss Nelson, 24, kabla ya uhamisho wa majira ya joto. (Football Insider)
Brighton pia wanaendelea kumtaka Kiernan Dewsbury-Hall wa Leicester City baada ya kushindwa katika ombi la Januari la kumnunua kiungo huyo Mwingereza, 25. (Talksport)
Inter Milan wana imani kwamba mshambuliaji wa Argentina Lautaro Martinez, 26, atasaini mkataba mpya. (Fabrizio Romano)
Mshambulizi wa Ufaransa Olivier Giroud, 37, anataka kuhamia Los Angeles au New York mkataba wake na AC Milan utakapokamilika mwishoni mwa msimu huu. (Gazzetta dello Sport – In Itali)
Liverpool wanamfuatilia kwa karibu beki wa Ajax mwenye umri wa miaka 18 na Uholanzi Jorrel Hato. (Football Insider)
Manchester City wako kwenye mazungumzo ya juu zaidi ya kumsajili mshambuliaji chipukizi wa Marekani Cavan Sullivan, 14, ambaye ni sehemu ya akademi ya Philadelphia Union lakini bado hajasaini mkataba wa kitaaluma. (Subscription Required)
BBC



