Transfer - International

Tetesi za usajili ulaya, Jumatano, March 20 2024

Joel JJ By Joel JJ
β€’
20 Mar 2024
Tetesi za usajili ulaya, Jumatano, March 20 2024

Mmiliki mwenza wa Manchester United Sir Jim Ratcliffe amemfanya meneja wa England Gareth Southgate chaguo lake kuu kuchukua nafasi ya Erik ten Hag msimu wa joto, na angependa uamuzi kutoka kwa mchezaji huyo wa miaka 53 mapema kuliko baadaye. (Star)

Manchester City huenda ikamruhusu winga wa Uingereza Jack Grealish, 28, kuondoka msimu huu wa joto huku wakitafuta pesa za kuboresha kikosi chao. (HITC)

Mshambulizi wa Newcastle United na Uswidi Alexander Isak, 24, yuko kwenye orodha ya walioteuliwa na Arsenal huku The Gunners wakilenga kuleta mshambuliaji wakati wa majira ya joto. (Football Insider)

Arsenal pia wanavutiwa na mshambuliaji wa Sporting Lisbon na Uswidi Viktor Gyokeres, 25. (Teamtalk)

Tottenham, Chelsea na West Ham zote zimeonyesha nia ya kutaka kumsajili mshambuliaji wa Uingereza Ivan Toney, 28, huku akiendelea kuvutia macho (Sun)

Mshambuliaji wa Ujerumani Timo Werner, 28, anataka Tottenham kuamsha chaguo la kumsajili kabisa msimu huu wa joto kwa euro 17m kutoka kwa klabu mama ya RB Leipzig. (Florian Plettenberg)

Kiungo wa kati wa Denmark Christian Eriksen, 32, amemwambia meneja wa Manchester United Erik ten Hag kwamba hajafurahishwa na kukosa muda wa kucheza. (Tipsbladet)

Aliyekuwa mkuu wa uajiri wa Chelsea Scott McLachlan analengwa na Newcastle kuchukua nafasi ya mkurugenzi wa michezo Dan Ashworth, ambaye anaelekea Manchester United. (Team Talks)

Rangers wako tayari kukubali pauni milioni 15 kumnunua mlinda mlango wa Uingereza Jack Butland, 31, huku nia ya kutaka kucheza Ligi Kuu ya Uingereza ikiongezeka. (Football Insider)

Everton, Nottingham Forest na West Ham wanamfuatilia winga Mwingereza Karamoko Dembele, 21, ambaye amefanya vyema msimu huu baada ya kujiunga na Blackpool kwa mkopo kutoka klabu ya Ufaransa ya Brest. (HITC)

Rufaa ya Nottingham Forest dhidi ya kukatwa kwao pointi nne kwa kukiuka sheria za kifedha inaweza kuhatarisha adhabu kuongezwa. (Times Saa – Subscription Required)

Nottingham Forest italazimika kumuuza mmoja wa wachezaji wake nyota kufikia mwisho wa Juni ili kuepuka kukatwa pointi nyingine kwa kukiuka sheria za kifedha msimu ujao. (Times – Subscription Required)

Mshambulizi wa Ubelgiji Johan Bakayoko anavutia Chelsea, Liverpool, Manchester City na Paris St-Germain, huku PSV Eindhoven ikitaka euro 50-60m kwa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 20. (Sky Sports Germany)

Mshambulizi wa Manchester City Erling Haaland, 23, ameipa klabu yake hofu kwa kuchechemea kutoka kwenye mazoezi akiwa kwenye majukumu ya kimataifa na Norway. (Guardian)

BBC

More Stories

Klopp amchagua ter stegen, kipa namba moja ujerumani
Klopp amchagua ter stegen, kipa namba moja ujerumani
3m ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
32m ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
1h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
1h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
2h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
3h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
3h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
16h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
18h ago
READ MORE β†’