Tetesi za usajili Ulaya, Jumatatu March 25 2024

Joel JJ By Joel JJ β€’ 25th March 2024


Tetesi za usajili Ulaya, Jumatatu March 25 2024

Manchester City wanafuatilia matukio yanayomhusu beki wa kati wa Everton Jarrad Branthwaite, huku Manchester United, Tottenham na Real Madrid pia wakimtaka Mwingereza huyo mwenye umri wa miaka 21. (Mail)

Manchester United imekuwa ikihusishwa na kumuuza kiungo wa kati wa Scotland Scott McTominay, lakini klabu hiyo inapanga kusalia na mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 27 na kumpa mkataba ulioboreshwa (Star)

Manchester United inamlenga kiungo wa kati wa Benfica na Ureno Joao Neves, 19, kama mojawapo ya vipaumbele vyao msimu wa joto, lakini klabu hiyo inaweza pia kufikiria kumnunua mchezaji wa kimataifa wa Ufaransa Adrien Rabiot, 28, anayechezea Juventus, kama chaguo wanaloweza kumudu(Caught Offside)

West Ham wanapanga kumnunua mshambuliaji wa Brentford na England Ivan Toney, 28, ambaye amekuwa akihusishwa na Arsenal na Chelsea. (Football Insider)

Tottenham wanaandaa dau la mapema la msimu wa kiangazi la kati ya £30m-£40m kumnunua kiungo wa kati wa Uingereza Conor Gallagher, 24, ambaye mkataba wake na Chelsea unamalizika 2025. (Football Insider)

Bayern Munich wanataka uamuzi kutoka kwa beki wa kushoto wa Kanada Alphonso Davies wiki ijayo kuhusu iwapo mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 23, ambaye anahusishwa na Real Madrid , atakubali mkataba mpya.(Sky Sports Germany)

Mshambuliaji wa Genoa Albert Gudmundsson yuko kwenye rada ya Tottenham, wakati Inter Milan pia wanavutiwa na mchezaji huyo wa kimataifa wa Iceland, 26.(Football Transfers)

Lakini Gudmundsson angependelea kusalia Italia na anatamani zaidi kujiunga na Inter, ingawa Juventus pia wanamfuatilia kwa karibu. (La Gazzetta dello Sport - kwa Kiitaliano)

Julian Nagelsmann, 36, alisema "haiwezekani" kwamba aongeze mkataba wake kama meneja wa Ujerumani hadi mwisho wa michuano ya Euro 2024 msimu huu wa joto, na mazungumzo kuhusu mkataba mpya yamefanyika. (Metro)

Manchester United inaweza kujaribu kumsajili beki wa Senegal Mikayil Faye mwenye umri wa miaka 19 kutoka Barcelona katika majira ya joto (Mail)

Rui Pedro Braz wa Benfica yuko juu kwenye orodha ya warithi wanaotarajiwa kuchukua mikoba ya Dan Ashworth kama mkurugenzi wa michezo wa Newcastle United . (Times - usajili unahitajika)

BBC


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.