Uongozi wa Simba umethibitisha kuwa klabu ya Al Ahly itawasili nchini Jumatano, March 27 siku mbili kabla ya mchezo dhidi ya Simba
Mchezo huo wa mkondo wa kwanza robo fainali ya ligi ya mabingwa barani Afrika utapigwa Ijumaa March 29 katika uwanja wa Benjamin Mkapa
Al Ahly wanatarajiwa kutua nchini kwa usafiri wa ndege binafsi
Ahmed aita mashabiki kwa Mkapa
Katika hatua nyingine, Meneja wa Habari na Mawasiliano klabu ya Simba Ahmed Ally amewataka mashabiki kutumia siku chache zilizobaki kununua tiketi ili kuhakikisha wanaujaza uwanja wa Benjamin Mkapa
"Sasa tumeingia Wiki ya maamuzi, maamuzi ya kununua tiketi kwa ajili ya mchezo wetu dhidi ya Al Ahly," alindika Ahmed katika ukurasa wake wa mtandao wa kijamii
Wakati tiketi za Platinum, Tanzanite na VIP A zikiwa zimemalizika, kasi ya manunuzi ya tiketi za madaraja mengine imekuwa ndogo
Matarajio ni kuwa kasi hiyo itaongezeka kuanzia leo na pengine katika siku zilizobaki Wanamsimbazi watachangamkia tiketi zote ili kujaza dimba la Mkapa



