Tetesi za soka Ulaya Jumatano, March 27 2024

Joel JJ By Joel JJ β€’ 27th March 2024


Tetesi za soka Ulaya Jumatano, March 27 2024

Mshambulizi wa Manchester City na Norway Erling Haaland ameonekana kulengwa na Barcelona katika msimu wa joto wa 2025. Wakala wa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 23, Rafaela Pimenta, alikutana na mkurugenzi wa michezo wa klabu hiyo ya La Liga, Deco, mwezi uliopita. (Mundo Deportivo - kwa Kihispania)

Mshambulizi wa Brentford na England Ivan Toney, 28, anaweza kuwa chaguo kwa Manchester United msimu huu wa joto. (Fabrizio Romano kupitia Caught Offside)

United wamemtambua kiungo wa kati wa Wolves wa Brazil Joao Gomes, 23, kama mbadala wa Casemiro, 32. (Sport - kwa Kihispania).

Arsenal inaonekana kuimarika katika nafasi yao ya kumsajili mshambuliaji wa Newcastle na Uswidi Alexander Isak baada ya mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 24 kukiri "mambo yanaweza kutokea" katika dirisha la usajili(Mail)

The Gunners wanafikiria kumnunua mlinzi wa kati wa Sporting Lisbon na Ivory Coast Ousmane Diomande, 20, baada ya kushuhudia makali yake katika safari ya kumtazama mshambuliaji wa Uswidi Viktor Gyokeres, 25. (Sun).

Gyokeres amempita mshambuliaji wa England na Brentford, Ivan Toney kwenye orodha ya washambuliaji wapya wanaotarajiwa kuwa wa Arsenal , huku West Ham pia wakimtaka. (TalkSport) Manchester United italeta kikosi kizima cha kiufundi cha England ikiwa watamteua Gareth Southgate kama meneja katika msimu wa joto.(Sun)

Lakini United wanataka kuzungumza na meneja wa Wolves Gary O'Neil kuhusu jukumu katika safu mpya ya ukufunzi huko Old Trafford. (ESPN)

Meneja wa zamani wa Chelsea, Manchester United na Tottenham Jose Mourinho anasema yuko tayari kurejea kufundisha msimu huu wa joto kufuatia kuondoka kwake kutoka Roma. (Fabrizio Romano)

Pamoja na wote wanaomtaka meneja wa Bayer Leverkusen Xabi Alonso, Liverpool na Bayern Munich wanamtaka kocha wa Brighton Roberto de Zerbi kama mbadala wake. (Bild - kwa Kijerumani)

Babake Luis Diaz anasema "tumaini bado halijapotea" kuhusu winga huyo wa Liverpool wa Colombia, 27, anayecheza Uhispania. (Cadena SER - kwa Kihispania)

Wolves wanaongoza katika kinyang'anyiro cha kumsajili mshambuliaji wa Southampton na Scotland Che Adams, 27, atakapokuwa mchezaji huru msimu wa joto. (Telegraph - usajili unahitajika)

Ajax wanachunguza mpango wa kumnunua kiungo wa kati wa Aston Villa Mwingereza Tim Iroegbunam, 20. (Football Insider) Sturm Graz anataka kumsajili mshambuliaji wa Arsenal na Denmark U21 Mika Biereth, 21, kwa mkataba wa kudumu kufuatia kipindi kizuri cha mkopo. (Evening Standard)

The Gunners wako tayari kumuuza beki wa pembeni wa Ureno Nuno Tavares, 24, msimu huu wa joto, huku Lazio ikivutiwa na huduma zake (Football London)

Chelsea itasikiliza ofa kwa kiungo wa kati wa Uingereza Conor Gallagher, 24, na mlinzi Trevor Chalobah, 24, pamoja na mshambuliaji wa Albania Armando Broja mwenye umri wa miaka 22 msimu huu wa joto huku wakijaribu kuepuka kukiuka kanuni za kifedha za Premier League. (Football Insider)

Brighton wanamfuatilia winga wa Nigeria Philip Otele, 24, ambaye anachezea klabu ya Cluj ya Romania . (Evening Standard) Real Madrid ilituma maskauti kumwangalia kiungo wa kati wa River Plate Muargentina Franco Mastantuono, 16.(90min)

BBC


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.