Tetesi za usajili Ulaya, Alhmisi March 28 2024

Joel JJ By Joel JJ β€’ 28th March 2024


Tetesi za usajili Ulaya, Alhmisi March 28 2024

Arsenal ina orodha ya wachezaji 10 wanaowania nafasi ya mshambuliaji mpya msimu huu wa joto huku Mslovenia wa RB Leipzig Benjamin Sesko, 20, Viktor Gyokeres wa Sporting Lisbon , 25, na mchezaji mwenzake wa kimataifa wa Uswidi, Alexander Isak, 24, wa Newcastle , wakiwa miongoni mwa wale wanaofuatiliwa.(Mirror)

Manchester United wanamtaka beki wa kati wa Everton Jarrad Branthwaite, 21, huku wakiweka kipaumbele katika kuboresha safu yao ya ulinzi msimu ujao. (Telegraph)

Pep Guardiola "anavutiwa" na kiungo wa Newcastle Bruno Guimaraes, 26, lakini Manchester City italazimika kulipa euro 100m (£85.7m) ili kumsajili mchezaji huyo wa kimataifa wa Brazil. (Fichajes - kwa Kihispania) West Ham wanatarajia Manchester City kutaka tena huduma za kiungo wao wa kati wa Brazil Lucas Paqueta, 26. (Football Insider)

Mshambulizi wa Liverpool Luis Diaz, 27, hajakata tamaa ya kuhamia moja ya vilabu vikubwa vya Uhispania La Liga siku zijazo, kulingana na babake mchezaji huyo wa kimataifa wa Colombia. (Daily Mail)

Chelsea ni miongoni mwa vilabu vinavyomhitaji mlinda lango wa Athletico Paranaense Bento, 24, ambaye alicheza mechi yake ya kwanza Brazil dhidi ya England wiki iliyopita. (Globo - kwa Kireno)

Tottenham wanataka kumsajili mshambuliaji wa Feyenoord wa Mexico Santiago Gimenez, 22, kama mbadala wao wa Harry Kane msimu huu wa joto - mwaka mmoja baada ya mshambuliaji huyo wa Uingereza mwenye umri wa miaka 30 kuondoka kwenda Bayern Munich(Caught Offside)

Manchester United wana nia ya kumsajili beki wa Argentina Aaron Anselmino, 18, kutoka Boca Juniors . (Ole - kwa Kihispania)

Kiungo wa kati wa Italia Jorginho, 32, anaweza kuondoka Arsenal msimu huu na kurejea katika nchi yake.(Football London)

Tottenham , West Ham , Brighton na Everton wote wanapanga kumsajili winga wa Juventus na England aliye katika kikosi cha chini ya umri wa miaka 21 Samuel Iling-Junior, 20. (Football Insider)

Matumaini ya The Gunners kumsajili winga Xavi Simons, 20, yamekwama kwa sababu Paris St-Germain wanataka kumpa mchezaji huyo wa kimataifa wa Uholanzi muda zaidi wa kucheza atakaporejea kutoka kwa mkopo RB Leipzig . (Express)

Meneja wa Brighton Roberto de Zerbi ndiye mgombea mkuu wa usimamizi wa Bayern Munich ikiwa hawawezi kumshawishi kiungo wao wa zamani Xabi Alonso kujiunga kutoka Bayer Leverkusen . (Florian Plettenberg)

Manchester United itamruhusu kiungo wa kati wa Denmark Christian Eriksen, 32, kuondoka msimu huu wa joto. (Football Insider)

Real Madrid hawawezi kumudu kumnunua beki wa pembeni wa Liverpool na Uingereza Trent Alexander-Arnold, 25. (Goal)

Kiungo wa kati wa Ujerumani Toni Kroos, 34, anatazamiwa kusaini mkataba wa mwaka mmoja kusalia Real Madrid . (Fabrizio Romano) Kocha msaidizi wa Liverpool Pep Lijnders atawania kuinoa Ajax msimu ujao. (Telegraph - usajili unahitajika)

BBC


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.