Mchezo wa kwanza wa robo fainali ligi ya mabingwa kati ya Simba dhidi ya Al Ahly umemalizika kwa wageni kuibuka na ushindi wa bao 1-0
Bao la dakika ya 5 lilifungwa na Ahmed Kouka lilidumu hadi dakika 90 za mchezo huo
Simba ilitengeneza nafasi nyingi katika mchezo huo lakini changamoto katika umaliziaji imeikosesha Simba matokeo mazuri leo
Ni mlima mrefu kwa Simba kwani ili kuweza kutinga nusu fainali itahitaji kushinda angalau mabao 2 katika mchezo wa marudiano utakaopigwa Misri wiki ijayo
Hakuna jambo lisilowezekana katika mpira wa miguu