Mechi ya kibabe kati ya Yanga dhidi ya Mamelodi Sundowns imemalizika uwanja wa Benjamin Mkapa kwa matokeo ya suluhu ya bila kufungana
Licha ya kuwakosa nyota wake muhimu, Kocha Mkuu wa Yanga Miguel Gamondi aliwabadilishia mbinu Mamelodi akitumia mashambulizi ya kushitukiza zaidi
Ni Yanga iliyotengeneza nafasi nyingi zaidi na pengine Wananchi wangeweza kuondoka na ushindi kama Kennedy Musonda, Aziz Ki na Clement Mzize wangetumia vyema baadhi ya nafasi walizopata
Ni lazima tuwape pongezi wachezaji wa Yanga kwani leo walicheza kwa nidhamu kubwa dhidi ya timu bora barani Afrika kwa sasa
Dakika nyingine 90 zitakwenda kupigwa huko Afrika Kusini wiki ijayo Yanga ikiingia katika mchezo huo ikiwa na cleansheet
Pengine wachezaji Khalid Aucho, Pacome Zouzoua na Yao Kouassi watakuwa tayari kurejea katika mchezo huo



