Yanga, Mamelodi Sundowns hakuna mbabe

Joel JJ By Joel JJ β€’ 30th March 2024


Yanga, Mamelodi Sundowns hakuna mbabe

Mechi ya kibabe kati ya Yanga dhidi ya Mamelodi Sundowns imemalizika uwanja wa Benjamin Mkapa kwa matokeo ya suluhu ya bila kufungana

Licha ya kuwakosa nyota wake muhimu, Kocha Mkuu wa Yanga Miguel Gamondi aliwabadilishia mbinu Mamelodi akitumia mashambulizi ya kushitukiza zaidi

Ni Yanga iliyotengeneza nafasi nyingi zaidi na pengine Wananchi wangeweza kuondoka na ushindi kama Kennedy Musonda, Aziz Ki na Clement Mzize wangetumia vyema baadhi ya nafasi walizopata

Ni lazima tuwape pongezi wachezaji wa Yanga kwani leo walicheza kwa nidhamu kubwa dhidi ya timu bora barani Afrika kwa sasa

Dakika nyingine 90 zitakwenda kupigwa huko Afrika Kusini wiki ijayo Yanga ikiingia katika mchezo huo ikiwa na cleansheet

Pengine wachezaji Khalid Aucho, Pacome Zouzoua na Yao Kouassi watakuwa tayari kurejea katika mchezo huo


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.