Mshambuliaji wa Azam FC aliyeaga klabuni hapo Prince Mpumelelo Dube amefungua malalamiko TFF akidai hakusaini mkataba mpya zaidi ya mkataba ambao unaisha mwishoni mwa msimu
Inadaiwa kuwa mshambuliaji huyo ameukana mkataba ambao Azam FC wanasema aliusaini na unaisha mwezi Juni 2026
Mshambuliaji huyo ametinga TFF na mkataba ambao anasema ni halali ambao unafikia ukomo wake mwisho mwa msimu huu yaani Juni 2024
Mshambuliaji huyo amepeleka nyaraka mbalimbali pamoja na vielelezo vingine kuthibishisha kuwa mkataba wake halali unatamatika mwishoni mwa msimu huu
Hivi karibuni mchezaji huyo aliwaaga Azam kupitia akaunti yake ya Instagram huku akiwashukuru watu mbalimbali katika klabu hiyo kama viongozi wa timu, idara mbalimbali pamoja na mashabiki wa klabu hiyo
Klabu ya Azam ilijibu mapigo Kwa kusema mshambuliaji huyo bado ni mchezaji wao kwani anao mkataba mrefu mpaka 2026
Klabu hiyo imeenda mbali na kumwambia mchezaji huyo kuwa kama anataka kuondoka afuate utaratibu wa kuvunja mkataba na sio kuaga akiwa bado ni mali yao
Kwa kujibu wa klabu hiyo ni kwamba thamani ya kuvunja mkataba wa mchezaji huyo ni 700m hivyo afike mezani na atimize matakwa ya kifungu hicho ili wamuachie huru
Azam FC imekuwa ikimuandikia barua mshambuliaji huyo kila baada ya siku tatu ikimhitaji aripoti kazini kuendelea na majukumu yake.



