Aziz Ki mchezaji bora wa ligi kuu March

Joel JJ By Joel JJ β€’ 2nd April 2024


Aziz Ki mchezaji bora wa ligi kuu March

Kiungo mshambuliaji wa Yanga Stephane Aziz Ki amechaguliwa kuwa mchezaji bora wa ligi kuu ya NBC kwa mwezi March 2024

Aziz Ki amebeba tuzo hiyo akiwashinda Feisal Salum wa Azam Fc na Clatous Chama wa Simba

Katika mwezi March, Aziz Ki alihusika katika mabao saba ya Yanga akifunga matatu na kutoa pasi nne za mabao

Aliisaidia Yanga kushinda mechi tatu kati ya nne walizocheza katika mwezi huo

Tuzo ya kocha bora wa mwezi imechukuliwa na Bruno Ferry wa Azam Fc


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.