Kiungo mshambuliaji wa Yanga Stephane Aziz Ki amechaguliwa kuwa mchezaji bora wa ligi kuu ya NBC kwa mwezi March 2024
Aziz Ki amebeba tuzo hiyo akiwashinda Feisal Salum wa Azam Fc na Clatous Chama wa Simba
Katika mwezi March, Aziz Ki alihusika katika mabao saba ya Yanga akifunga matatu na kutoa pasi nne za mabao
Aliisaidia Yanga kushinda mechi tatu kati ya nne walizocheza katika mwezi huo
Tuzo ya kocha bora wa mwezi imechukuliwa na Bruno Ferry wa Azam Fc




