Klabu ya Yanga imeanza mazungumzo ya kumuongeza mkataba kiungo mshambuliaji Stephane Aziz Ki ambaye mkataba wake unamalizika mwishoni mwa msimu
Aziz Ki amekuwa na kiwango bora msimu huu akiwa kinara wa mabao katika ligi kuu ya NBC akifunga mabao 13 na kutoa pasi saba za mabao
Ni wazi ubora huo umezivutia timu nyingi ikiwemo klabu ya Mamelodi Sundowns ambayo inatajwa kuanza juhudi za chinichini kumshawishi nyota huyo raia wa Burkina Faso akajiunge nao
Ni baada ya kuwasumbua katika mechi mbili za robo fainali ligi ya mabingwa ambapo kocha wa Sundowns Rulani Mokwena alionekana kuvutiwa na uwezo wake. Mokwena alionekana kufanya mazungumzo na Aziz Ki baada ya mechi zote mbili
Hata hivyo Yanga iko katika nafasi nzuri ya kumbakisha kwa kuwa Aziz Ki mwenyewe anafurahia maisha yake na mabingwa hao wa Tanzania Bara
Aziz Ki ameweka wazi kuwa bado hajamaliza kazi iliyomleta Yanga hivyo hafikirii kuondoka kwa sasa na hakuna thamani yoyote ya pesa inayoweza kumshawishi



