Klabu za Simba na Azam Fc zitaiwakilisha Tanzania Bara katika michuano maalum ya Muungano itakayopigwa kuanzia Jumatano, April 24 uwanja wa New Amaan Complex, visiwani Zanzibar
Azam Fc wamechukua nafasi ya Yanga ambayo ilipaswa kushiriki kwa kuwa mabingwa wa Tanzania Bara sambamba na Simba iliyomaliza nafasi ya pili msimu uliopita
Kulingana na ratiba iliyotolewa na TFF na ZFF, mechi za nusu fainali zitapigwa April 24 ambapo Simba itachuana na KVZ wakati Azam Fc wakichuana na KMKM
Mchezo wa fainali utapigwa April 27 simu moja baada ya shamrashamra za Muungano, April 26




