Ratiba ya Simba, May 2024 usipime!

Joel JJ By Joel JJ β€’ 2nd May 2024


Ratiba ya Simba, May 2024 usipime!

Ligi Kuu ya NBC inafikia tamati May 28 ambapo katika siku 26 Simba itapaswa kucheza mechi nane

Ni mchaka-mchaka wa aina yake kwani Mnyama atashuka dimbani kila baada ya siku tatu hadi nne

April 30 Simba ilikuwa Ruangwa kumenyana na Namungo Fc na kesho May 03 itakuwa uwanja wa Azam Complex kumenyana na Mtibwa Sugar

Baada ya siku tatu tena, Smba itarudi tena Azam Complex kumenyana na Tabora United. Ni siku tatu nyingine zitapita kabla ya kuelekea uwanja wa Benjamin Mkapa kumenyana na Azam Fc katika mchezo ambao Simba itahitaji ushindi ili kuiondoa Azam Fc katika nafasi ya pili


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.