Mchezo wa pili wa nusu fainali kombe la Shirikisho la CRDB Bank kati ya Ihefu Fc dhidi ya Yanga umepangwa kupigwa mkoani Arusha, May 19 katika uwanja wa Sheikh Amri Abeid
Ni katika uwanja uleule ambao Yanga ilitwaa taji hilo msimu uliopita kwa kuichapa Azam Fc bao 1-0 kwenye mchezo wa fainali
Mchezo wa kwanza wa nusu fainali kati ya Coastal Union dhidi ya Azam Fc utapigwa May 18 katika uwanja wa CCM Kirumba, Mwanza

Mechi ya fainali inatarajiwa kupigwa Juni 02



