Bado Simba ina matumaini ya kumshawishi kiungo mshambuliaji Kibu Denis kusaini mkataba mpya kuendelea kuwatumikia Wekundu hao wa Msimbazi
Habari kutoka ndani ya uongozi wa Simba zimethibitisha kuwa wiki ijayo, watakutana na wakala wa Kibu ili kumaliza mvutano uliopo juu ya mkataba mpya
Kibu bado hajasaini mkataba aliopatiwa na Simba akitaka dau nono zaidi ambalo hata hivyo kiuhalisia anaweza kukwama kwani kiasi cha Tsh Milioni 500 alizohitaji ni fedha nyingi sana kwa mkataba wa miaka miwili
Wakati Kibu anasajiliwa na Simba misimu miwili iliyopita kutoka klabu ya Mbeya City, Simba ilitumia Tsh Milioni 200 kumsajili ambapo sehemu ya fedha hizo ililipwa Mbeya City ambayo ilikuwa bado ina mkataba wa mwaka mmoja na Kibu
Aidha baada ya kukamilisha usajili wake, uongozi wa Simba ulipambana kuhakikisha Kibu anapata uraia wa Tanzania na hivyo kusajiliwa kama mchezaji wa ndani
Rais wa heshima klabu ya Simba Bilionea Mohamed Dewji ametaka Kibu aendelee kubaki Msimbazi hivyo baada ya mazungumzo hayo hatma yake itafahamika



