Stars yaalikwa Saudi Arabia

Joel JJ By Joel JJ β€’ 7th May 2024


Stars yaalikwa Saudi Arabia

Timu ya Taifa ya Tanzania 'Taifa Stars' imealikwa Saudi Arabia kushiriki michuano maalum ambapo itacheza mechi za Kimataifa za kirafiki dhidi ya Sudan

Mapema leo Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) liliweka hadharani majina ya wachezaji katika kikosi kitakachosafiri Jumatano, May 08 2024

Kikosi hicho hakijamuisha nyota wa klabu za Yanga, Azam Fc na Simba ambazo zimewekeza nguvu katika mechi za kuhitimisha msimu wa ligi kuu ya NBC

Hata hivyo Simba imemruhusu mlinda lango wake Ali Salim kujiunga na kikosi hicho


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.