Simba yajipanga na vita ya nafasi ya pili

Joel JJ By Joel JJ β€’ 14th May 2024


Simba yajipanga na vita ya nafasi ya pili

Meneja wa Habari na Mawasiliano klabu ya Simba Ahmed Ali amewapa pole Wanasimba wote baada ya jitihada za kuwania ubingwa ligi kuu msimu huu kufika tamati jana

Ahmed amesema licha ya machungu wanayopitia, hawapaswi kukata tamaa kwani mechi nne zilizobaki ni muhimu sana katika kuhakikisha wanamaliza katika nafasi ya pili

Ahmed amesema Simba lazima ijihakikishie tiketi ya kucheza ligi ya mabingwa msimu ujao kwani kama wataikosa nafasi hiyo maumivu yatakuwa makali zaidi

Kupitia ukurasa wake wa mtandao wa kijamii, Ahmed ameandika ujumbe huu;

"Leo ni usiku mgumu kwetu uliojaa maumivu na uchungu mkali

Lakini hatuna budi kukubali kuwa huu ndio ushindani

Kitu muhimu wana Simba ni kutambua kuwa kwetu ligi haijaisha

Tungali bado mioyo yetu inavuja damu kwa uchungu wa kukosa taji lakini hatuna budi kusimama imara tuipiganie Simba yetu imalize nafasi ya pili

Hii ndio nafasi pekee yenye thamani tuliyobakiwa nayo kwa sasa, inawezekana usione uzito wa nafasi hiyo lakini tukiiikosa ndio utagundua tumepoteza kitu kikubwa kiasi gani

Lets go wana Simba kila vita ina hatua zake tumepoteza hatua ya kwanza sasa tupambane tushinde ya hatua pili

Tukifanikiwa kushinda vita ya hatua ya pili, turudi kambini tujipange kuanza upya kwa msimu ujao"


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.