Tetesi za usajili Ulaya, Jumanne May 14 2024

Joel JJ By Joel JJ β€’ 14th May 2024


Tetesi za usajili Ulaya, Jumanne May 14 2024

Klabu za Ligi Kuu ya Saudia (Saudi Pro) zina nia ya kumsajili kiungo wa kati wa Manchester United na Brazil Casemiro, 32, na kiungo wa kati wa Ureno mwenye umri wa miaka 29 Bruno Fernandes. (Telegraph - usajili unahitajika)

Arsenal wanakaribia kumpoteza mlinzi Reuell Walters, 19, baada ya mchezaji huyo wa kimataifa wa Uingereza wa wachezaji wa chini ya miaka 20 kukataa ofa ya kandarasi mpya ili kutafuta nafasi kwingineko. (Athletic- Usajili unahitajika)

Real Madrid bado wana nia ya kumsajili mchezaji wa kimataifa wa Uingereza Trent Alexander-Arnold, 25, kutoka Liverpool. (Fabrizio Romano kupitia Football365)

Ripoti za mzozo kuibuka kwa mkubwa kati ya mshambuliaji wa Ufaransa Kylian Mbappe, 25, na rais wa Paris St-Germain Nasser Al-Khelaifi kabla ya mechi ya Ligue 1 dhidi ya Toulouse zimetupiliwa mbali na vyanzo vya mabingwa hao wa Ufaransa. (Marca kwa Kihispania)

Kocha wa Bayer Leverkusen Xabi Alonso anatumai kusimamia klabu zake zote tatu za zamani za Liverpool, Real Madrid na Bayern Munich lakini hana uhakika ni kwa utaratibu gani. (Abendzeitung - kwa Kijerumani)

Nia ya Bayern Munich kumnunua mkufunzi wa Crystal Palace Oliver Glasner ilififia baada ya klabu hiyo ya Bundesliga kuambiwa itawagharimu pauni milioni 86 ili kumzawadia kutoka Selhurst Park. (Bild - kwa Kijerumani - usajili unahitajika)

Napoli wameanzisha tena mazungumzo na Antonio Conte kuhusu kuwa meneja wao baada ya Muitaliano huyo kupunguza mahitaji yake ya mshahara, huku AC Milan pia ikitaka kuzungumza na kocha huyo wa zamani wa Chelsea na Tottenham. (Il Mattino - kwa Kiitaliano - usajili unahitajika)

Mlinzi wa zamani wa Sevilla na timu ya taifa ya Uhispania Sergio Ramos, 38, amepiga hatua katika mazungumzo yake klabu ya San Diego FC kuhusu kuhamia Ligi Kuu ya Soka (MLS) (Athletic - Usajili unahitajika)

Beki wa zamani wa timu ya taifa ya Uingereza, klabu za ligi kuu ya England Arsenal na Chelsea Ashley Cole, 43, ananyatiwa na klabu kadhaa vya Championship ili kuchukua nafasi ya kocha. (Mirror)

Chelsea wanatazamia kusajili mshambuliaji na mabeki wawili msimu huu wa joto huku wakurugenzi wa michezo wa klabu hiyo Paul Winstanley na Laurence Stewart wakitarajiwa kukabidhiwa tena majukumu yao ya uhamisho. (Telegraph - usajili unahitajika)

Winga wa zamani wa Manchester United Nani, 37, anasaka klabu mpya baada ya mkataba wa Mreno huyo katika klabu ya Adana Demirspor ya Uturuki kuvunjwa. (Mirror)

Wachezaji kadhaa wa Manchester United hawajashawishika na uwezo wa Rasmus Hojlund wa kufunga mabao hivyo wamekuwa wakisita kumwekea pasi mshambuliaji huyo wa Denmark mwenye umri wa miaka 21 wakati wa mechi. (Manchester Evening News)

BBC


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.