Nahodha wa timu ya Taifa ya Tanzania, Mbwana Samatta ametwaa Ubingwa wa Ligi Kuu ya Ugiriki Msimu wa 2023/24
Hilo ni taji la kwanza kwa Samatta nchini humo tangu ajiunge na Paok FC mnamo Agosti 2022, baada ya kuondoka Aston Villa ya England
Aliondoka Aston Villa kwa mkopo kwenda Fenerbahçe ya Uturuki, baadae KRC Genk kabla ya kuhamia Paok FC. Soma
Haya ni mafanikio makubwa kwake baada ya yale aliyopata akiwa na KRC Genk
Paok Fc watashiriki michuano ya ligi ya mabingwa barani Ulaya msimu ujao na pengine itakuwa nafasi nyingine kwa Samatta kushiriki michuano hiyo




