Samatta abeba ubingwa Ugiriki

Joel JJ By Joel JJ β€’ 20th May 2024


Samatta abeba ubingwa Ugiriki

Nahodha wa timu ya Taifa ya Tanzania, Mbwana Samatta ametwaa Ubingwa wa Ligi Kuu ya Ugiriki Msimu wa 2023/24

Hilo ni taji la kwanza kwa Samatta nchini humo tangu ajiunge na Paok FC mnamo Agosti 2022, baada ya kuondoka Aston Villa ya England

Aliondoka Aston Villa kwa mkopo kwenda Fenerbahçe ya Uturuki, baadae KRC Genk kabla ya kuhamia Paok FC. Soma

Haya ni mafanikio makubwa kwake baada ya yale aliyopata akiwa na KRC Genk

Paok Fc watashiriki michuano ya ligi ya mabingwa barani Ulaya msimu ujao na pengine itakuwa nafasi nyingine kwa Samatta kushiriki michuano hiyo


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.