Jumamosi May 25 2024 mabingwa wa soka Tanzania Bara, Yanga watakabidhiwa kombe la Ligi Kuu ya NBC 2023/24 baada ya kufanikiwa kulitetea kwa msimu wa tatu mfululizo
Katika kufanya siku hiyo kuwa ya kipekee, NBC Bank wameandaa matukio ya aina yake jijini Dar es salaam
Akizungumza katika Mkutano wa pamoja na Wanahabari kati ya Yanga na NBC Bank, Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Yanga Ali Kamwe amesema Helkopta (chopa) maalum imeandaliwa kwa ajili ya kufanya paredi la ubingwa jijini Dar es salaam
"Kuanzia saa 5 asubuhi kutakuwa na Helkopta itakayofanya paredi ya ubingwa ndani ya Jiji la Dar es salaam"
"Hili litakuwa tukio la kwanza na la aina yake kufanyika hapa Afrika, sisi tunakwenda kuwafundisha namna ubingwa unasherehekewa"
"Baada ya kufanya parade maeneo mbalimbali, saa 9 Alasiri Helkopta itatua uwanja wa Benjamin Mkapa kuleta kombe"
"Yaani wakati mashabiki wa Yanga wakiwa tayari wameujaza uwanja wa Mkapa, Helkopta itatua, kombe litakabidhiwa kisha itaondoka," alisema Kamwe
Yanga ni mabingwa tangu Bank ya NBC ilipoanza kudhamini ligi kuu ya Tanzania Bara. Likiwa taji la tatu ambalo Yanga watakabidhiwa kuwa mali yao



