Mlinzi wa kati wa Coastal Union na timu ya Taifa ya Tanzania 'Taifa Stars' Lameck Lawi jana aliwaaga mashabiki wa Coastal Union baada ya mchezo wa ligi kuu dhidi ya KMC uliopigwa uwanja wa Mkwakwani
Baada ya dakika 90 za mchezo huo uliomalizika kwa matokeo ya suluhu ya bila kufungana, Lawi alionekana akiwapungia mashabiki huku akionesha huzunika kubwa kwani aliitumikia timu hiyo kwa mapenzi makubwa
Msimu huu Coastal Union wamemaliza nafasi ya nne na kujihakikishia tiketi ya kucheza michuano ya kombe la Shirikisho barani Afrika
Lawi alikuwa miongoni mwa wachezaji muhimu waliopambana kuhakikisha Coastal Union inafikia mafanikio hayo
Wengi wanamtabiria huenda akaibuka na tuzo ya beki bora wa ligi kuu ya NBC msimu huu
Tayari klabu ya Simba ilishamalizana na Coastal Union hivyo kituo kinachofuata kwa Lawi ni Msimbazi



