Bodi ya Wakurugenzi klabu ya Simba imewatangazia Wanachama wake kuwa inakaribisha maombi ya kazi ya mkataba nafasi ya Mkurugenzi wa Mashabiki na wanachama
Akizungumza kuhusu nafasi hii Afisa Mtendaji Mkuu wa Simba, Imani Kajula amesema;
"Hii ni nafasi muhimu sana katika klabu yetu hivyo tunakaribisha waombaji wenye vigezo vilivyotajwa hapo juu kuleta maombi yao ndani ya muda uliopangwa"
"Tumedhamiria kuimarisha Idara ya Wanachama na Mashabiki ili kuwapa Wanachama wetu huduma bora, kusogea karibu yao na kuboresha uandikishaji wanachama baada ya Katiba ya Simba kuondoa ukomo wa namba ya Wanachama"



