Ihefu sasa ni Singida Black Stars

Joel JJ By Joel JJ β€’ 6th June 2024


Ihefu sasa ni Singida Black Stars

Klabu ya Ihefu Fc ambayo kwa sasa makazi yake ni mkoani Singida, imetangaza mchakato wa kubadili jina umekamilika hivyo kwa sasa timu hiyo ifahamike kama SINGIDA BLACK STARS

Klabu hiyo imetoa taarifa kwa UMMA juu ya mabadiliko hayo;

"Tunaifahamu kwa jina la Singida Black Stars ambapo msimu ulioisha ilikuwa ikiitwa Ihefu Fc na hii ni baada ya kutangaza kuachana rasmi na jina la IHEFU SC baada ya mchakato wa mabadiliko ya usajili wa jina la Singida Black Stars kukamilika"

"Kuanzia sasa timu itafahamika kwa jina la Singida Black Stars SC na Makao Makuu ya Klabu yatakuwa mjini Singida,

"Mabadiliko haya ni sehemu ya maboresho muhimu yanayoendelea ndani ya klabu kuelekea maandalizi ya msimu wa mashindano 2024/2025.”


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.