Mfadhili wa zamani wa klabu ya Simba Azim Dewji amewataka Wanachama na Mashabiki kuwa watulivu na kutumia njia za kistaarabu kutatua changamoto zilizopo
Azim amesema haungi mkono shinikizo la mashabiki kwa baadhi ya viongozi kuwataka wajiuzulu kwani njia hiyo haiwezi kuwasaidia
"Mimi naamini Simba tulikuwa na timu nzuri msimu uliomalizika. Tumekosa nafasi ya pili kwa tofauti ya mabao tu lakini tumefunga pointi na Azam Fc hivyo naweza kusema na sisi ni wa pili"
"Lazima tukubali ushindani ulikuwa mkubwa, washindani wetu nao walikuwa wamejipanga, hatukuwa na timu mbaya"
"Tutumie njia za kistaarabu kutatua changamoto zilizopo, tusichukue maamuzi ya kukurupuka kwani tunaweza kuharibu," alisema Dewji
Aidha Dewji amewashauri viongozi wa Simba kujitokeza hadharani haraka kuwatuliza mashabiki huku akiwataka pia kuhakikisha wanasimamia vizuri usajili wa dirisha kubwa sambamba na kutafuta kocha ambaye atakaa kwa muda mrefu badala ya kuwa na mabadiliko ya mara kwa mara ambayo yamekuwa yakiiathiri timu



