Yanga - Local

Tamasha la Wape Tabasam kufanyika mkoani Morogoro

Joel JJ By Joel JJ
β€’
22 Jun 2024
Tamasha la Wape Tabasam kufanyika mkoani Morogoro

Mkoa wa Morogoro siku ya leo Jumamos utapata ugeni mkubwa kutoka maeneo mbalimbali ya nchi ambapo Wananchi watafurika kushuhudia Tamasha la Wape Tabasamu lililoandaliwa na nyota wa Yanga Kibwana Shomari na Dickson Job

Ni mechi ya 'charity' kwa ajili ya kuchangisha fedha ambazo zitakwenda kusaidia wale wenye changamoto mbalimbali

Ni msimu wa tatu Job na Kibwana wanaandaa Tamasha hili lakini mwaka huu linaonekana kuwa na mvuto zaidi

Ushindani ni mkali kuanzia katika usajili wa wachezaji lakini hata 'mabosi' nao kuchagua upande

GSM pamoja na Arafat Haji wao wamechagua upande wa Kibwana wakati Injinia Hersi Said yeye yuko upande wa Job

Wachezaji kama Pacome Zouzoua, Clatous Chama, Prince Dube wanatarajiwa kuitumikia timu Job wakati vinara wa mabao ligi kuu msimu uliopita Stephane Aziz Ki aliyekuwa mfungaji bora na Feisal Salum aliyeshika nafasi ya pili wako timu Kibwana bila kumsahau Mukoko Tonombe

Kumekuwa na matukio ya 'kuporana' wachezaji ambapo beki Ibrahim Bacca ambaye awali alitangaza kuwa timu Kibwana jana alionekana akisaini kuitumikia timu Job kwa kile alichoeleza timu Kibwana hawana hela!

Ni katika 'kunogesha' Tamasha hilo ambalo mafanikio yake yatapeleka Tabasamu kwa watu wengi zaidi

Kutakuwa na treni ya mwendokasi kutoka jijini Dar es salaam ambayo itapeleka mashabiki mkoani Morogoro na kuwarudisha Dar baada ya mchezo

Azam TV nao watakuwa mbashara Baraka Mpenja akipewa jukumu la kuhabarisha yatakayojiri dimba la Jamhuri kuanzia saa 10 jioni

More Stories

Klopp amchagua ter stegen, kipa namba moja ujerumani
Klopp amchagua ter stegen, kipa namba moja ujerumani
2m ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
31m ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
1h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
1h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
2h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
3h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
3h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
16h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
18h ago
READ MORE β†’