Muda mchache baada ya klabu ya Simba kutangaza kumsajili beki wa Coastal Union Lameck Lawi ambaye pia hucheza timu ya Taifa ya Tanzania 'Taifa Stars, klabu ya Coastal Union ikaibuka kukanusha usajili huo na kusisitiza Lawi bado ni mchezaji wao
Mwenyekiti wa Coastal Union Steven Mguto amesema klabu ya Simba haikufuata taratibu walizopewa na Coastal na hivyo kupelekea dili hilo kufa
Hata hivyo Mjumbe wa Bodi ya Wakurugenzi klabu ya Simba Crescentius Magori amesema Simba ilifuata taratibu ikiwa ni pamoja na kulipa fedha zote walizotakiwa walipe
Magori amedai sababu ya Coastal Union 'kugeuka' ni baada ya kupokea ofa kutoka klabu nyingine barani Ulaya
"Ndio tulichelewa kumaliza pesa,tulilipa nusu lakini mpaka June tulikuwa tumemaliza kulipa pesa yoye ya usajili, Tumemsajili Lameck Lawi kwa kufuata utaratibu, Wangesema kama ukichelewa kulipa mkataba unavunjika. Mpaka June tulikuwa tumemaliza kulipa pesa yote na nyaraka zote tunazo hata tukienda FIFA"
"Kilichotokea Coastal Union wamepata dili kutoka nje ndio maana wakabadili maamuzi," alisema Magori
Klabu ya Coastal Union imerejesha fedha zote walizolipwa nan Simba na kusisitiza hakuna biashara kati yao na Simba!



