Coastal Union - Local - Transfer

Coastal Union yamuwania Kisinda

Joel JJ By Joel JJ
β€’
22 Jun 2024
Coastal Union yamuwania Kisinda

Wakati ikianza kutangaza majina ya wachezaji inayowaacha, Coastal Union iko mbioni kumsajili winga wa zamani wa Yanga, Tuisila Kisinda, lengo ikiwa ni kujiimarisha kuelekea mashindano ya kimataifa ya Kombe la Shirikisho Afrika, imefahamika

Habari kutoka ndani ya Coastal Union zinasema mazungumzo na Kisinda yameshaanza, na endapo yakienda vyema, basi mchezaji huyo atamwaga wino katika klabu hiyo

"Tunaendelea na usajili, na tunalenga wachezaji ambao ni wazoefu kwenye michuano ya kimataifa, huwezi kwenda kucheza huku ukiwa na vijana wengi, wakongwe, siyo wa umri, ila kwenye mechi kubwa wanahitajika, hivyo tunamkata Kisinda, najua atakuja kutusaidia kwa sababu amecheza klabu kubwa kama AS Vita, Yanga na RS Berkane," kilisema chanzo

Siku chache kabla ya taarifa hizi, Ofisa Habari ya Klabu hiyo, Abbas El Sabri, alikiri kufanya mazungumzo ya mchezaji mwingine raia ya Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo (DRC), Djuma Shaaban

"Ni kweli tupo katika mazungumzo na Djuma, ni mchezaji mzuri, mzoefu katika mechi za kimataifa. Unajua tangu tulipopata nafasi ya kucheza Kombe la Shirikisho, tayari kama klabu tukatambua mahitaji yetu yataongezeka, kuanzia gharama, wachezaji na hata muda utakuwa finyu," alisema El Sabri

Mbali na huyo ambaye Coastal Union imekiri, lakini taarifa zinasema wanaendelea na mazungumzo na Saido Ntibazonkiza aliyeachwa na Simba hivi karibuni

More Stories

Klopp amchagua ter stegen, kipa namba moja ujerumani
Klopp amchagua ter stegen, kipa namba moja ujerumani
2m ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
31m ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
1h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
1h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
2h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
3h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
3h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
16h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
18h ago
READ MORE β†’