Bingwa mtetezi wa Kombe la Copa America, Argentina imeanza vyema kutetea taji hilo baada ya kuibuka na ushindi mabao 2-0 dhidi ya Canada katika mechi ya ufunguzi wa michuano hiyo hatua ya makundi
Argentina inasaka taji lake la tatu mfululizo baada ya kushinda Copa America ya 2021 na Kombe la Dunia la 2022 na imeanza kampeni hiyo kundi A katika uwanja wa Mercedes-Benz uliopo Atlanta, Georgia Marekani
Lionel Messi, ambaye atafikisha miaka 37 Juni 24, alitengeneza bao la kwanza alipopitisha pasi katikati ya walinzi wa Canada kwenda kwa Alexis Mac Allister aliyeupiga mpira kwa mguu wa kulia na Julian Alvarez kufunga dakia 49 huku akigongana na mlinda lango Maxime Crepea
Kisha Messi akatoa pasi ya bao la pili la Lautaro Martinez dakika ya 88. Messi amevunja rekodi ya Copa America kwa kucheza mechi yake ya 35, moja zaidi ya Sergio Livingstone wa Chile kuanzia mwaka 1941 hadi 1953. Messi ameendeleza rekodi yake mwenyewe kwa kutoa pasi ya 18



