Simba yafuata kiungo Rivers United

Joel JJ By Joel JJ β€’ 22nd June 2024


Simba yafuata kiungo Rivers United

Simba imerudi tena Nigeria katika klabu ya Rivers United ambapo iko mbioni kukamilisha usajili wa kiungo mkabaji Augustine Okejepha mwenye umri wa miaka 20

Kwa mujibu wa Mwanahabari maarufu wa Ghana Micky Jr, Okejepha amekubali kutua Msimbazi na atasaini mkataba wa miaka mitatu

Klabu ya Simba iko katika hatua za mwisho za mazungumzo kumalizana na Rivers United

Okejepha atakuwa Mnigeria wa nne kuitumikia Simba katika misimu ya karibuni baada ya Nelson Okwa, Victor Akpan na Junior Lokosa

Hata hivyo Lokosa, Akpan na Okwa walishindwa kuonesha makali yao katika kikosi cha Simba

Okejepha alikuwa moja ya wachezaji bora katika kikosi cha Rivers United msimu uliopita


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.