Simba imerudi tena Nigeria katika klabu ya Rivers United ambapo iko mbioni kukamilisha usajili wa kiungo mkabaji Augustine Okejepha mwenye umri wa miaka 20
Kwa mujibu wa Mwanahabari maarufu wa Ghana Micky Jr, Okejepha amekubali kutua Msimbazi na atasaini mkataba wa miaka mitatu
Klabu ya Simba iko katika hatua za mwisho za mazungumzo kumalizana na Rivers United
Okejepha atakuwa Mnigeria wa nne kuitumikia Simba katika misimu ya karibuni baada ya Nelson Okwa, Victor Akpan na Junior Lokosa
Hata hivyo Lokosa, Akpan na Okwa walishindwa kuonesha makali yao katika kikosi cha Simba
Okejepha alikuwa moja ya wachezaji bora katika kikosi cha Rivers United msimu uliopita



