Yanga yamshusha mrithi wa Lomalisa

Joel JJ By Joel JJ β€’ 7th July 2024


Yanga yamshusha mrithi wa Lomalisa

Mapema wiki hii Yanga ilithibitisha kuachana na mlinzi wa kushoto Joyce Lomalisa baada ya mkataba wake kumalizika

Yanga tayari imemshusha nchini mlinzi wa kushoto Chardack Boka nae kutoka DR Congo

Boka (24) alikuwa akiitumikia klabu ya FC Lupopo ya huko DR Congo, ndiye anayetarajiwa kurithi mikoba ya Lomalisa

Wakati Yanga ikitarajiwa kuanza maandalizi ya pre-season Avic Town hapo kesho, ni suala la muda kwa Boka na nyota wengine wapya waliosajiliwa kutambulishwa

Mpaka sasa Yanga imetambulisha wachezaji wawili wapya, Clatous Chama na Prince Dube

Taarifa za ndani ni kuwa bado kuna 'vyuma' vingine vitatu vinasubiri utambulisho


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.