Khomein atambulishwa Yanga

Joel JJ By Joel JJ β€’ 8th July 2024


Khomein atambulishwa Yanga

Klabu ya Yanga imethibitisha kukamilisha usajili wa mlinda lango Aboubakar Khomein kutoka klabu ya Ihefu Fc (Singida Black Stars)

Ni usajili uliokuwa ukisubiri utambulisho kwani Wananchi walikamilisha usajili huo majuma kadhaa nyuma

Khomein anatua Yanga kuchukua nafasi ya Metacha Mnata ambaye aliruhusiwa kuondoka baada ya mkataba wake kumalizika

Anajiunga kuimarisha eneo la golikipa ambalo tayari liko mikononi mwa Djigui Diarra na Aboutwalib Mshery

Khomein ni mlinda lango mwenye uzoefu na ligi ya Tanzania Bara pia akipata nafasi ya kuitumikia timu ya Taifa kuanzia ngazi ya vijana


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.