Jobe, Kanoute, Sarr kuachwa Simba

Joel JJ By Joel JJ β€’ 9th July 2024


Jobe, Kanoute, Sarr kuachwa Simba

Wakati kikosi cha Simba kikiondoka jana kuelekea Ismailia, Misri kwa ajili ya pre-season baadhi ya wachezaji hawajumuishwa katika msafara huo kwani hawako katika mipango ya Simba ya msimu ujao

Mshambuliaji Pa Omar Jobe ni miongoni mwa wachezaji ambao wamebaki uongozi ukiendelea kujadiliana nae kuhusu mustakabali wake

Simba imesajili washambuliaji wawili Steven Mukwala na Valentino Mashaka huku pia ikimbakisha Freddy Michael

Aidha viungo Sadio Kanoute na Babacar Sarr nao wanaelekea kupewa mkono wa kwaheri majadiliano yakiendelea

Simba imeimarisha zaidi safu ya kiungo kwa kuwasajili Augustine Okejepha, Debora Fernandez, Jean Ahoa na Yusuph Kagoma huku Mzamiru Yassin akiendelea kusalia


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.