Wakati kikosi cha Simba kikiondoka jana kuelekea Ismailia, Misri kwa ajili ya pre-season baadhi ya wachezaji hawajumuishwa katika msafara huo kwani hawako katika mipango ya Simba ya msimu ujao
Mshambuliaji Pa Omar Jobe ni miongoni mwa wachezaji ambao wamebaki uongozi ukiendelea kujadiliana nae kuhusu mustakabali wake
Simba imesajili washambuliaji wawili Steven Mukwala na Valentino Mashaka huku pia ikimbakisha Freddy Michael
Aidha viungo Sadio Kanoute na Babacar Sarr nao wanaelekea kupewa mkono wa kwaheri majadiliano yakiendelea
Simba imeimarisha zaidi safu ya kiungo kwa kuwasajili Augustine Okejepha, Debora Fernandez, Jean Ahoa na Yusuph Kagoma huku Mzamiru Yassin akiendelea kusalia



