Yanga imethibitisha usajili wa kiungo Aziz Andambwile kutoka klabu ya Singida FG
Andambwile anatua Jangwani kuziba nafasi iliyoachwa na Zawadi Mauya ambaye alipewa mkono wa kwaheri baada ya mkataba wake kumalizika
Kabla ya kujiunga na Singida FG, Andambwile alin'gara na kikosi cha Mbeya City
Amewahi kucheza soka la kulipwa nchini Malawi katika klabu ya Nyasa Big Bullets na pia kuzitumikia timu za Taifa za Malawi (U20) na Taifa Stars



