Gareth Southgate amejiuzulu nafasi ya Meneja wa Uingereza baada ya kushindwa katika fainali ya Euro 2024 na Uhispania
Uingereza ilichapwa mabao 2-1 na Uhispania juzi na kupoteza fainali ya pili mtawalia katika michuano ya Euro
Aidha mwaka 2018 timu hiyo pia ilitupwa nje ya michuano ya kombe la Dunia hatua ya nusu fainali
Ni takribani sasa miaka 58 Uingereza haijashinda taji la mashindano yoyote
Shirikisho la Mpira wa Miguu Uingereza FA limesema mchakato wa kumteua mrithi wake unaendelea



