Southgate amekubali yaishe

Joel JJ By Joel JJ β€’ 16th July 2024


Southgate amekubali yaishe

Gareth Southgate amejiuzulu nafasi ya Meneja wa Uingereza baada ya kushindwa katika fainali ya Euro 2024 na Uhispania

Uingereza ilichapwa mabao 2-1 na Uhispania juzi na kupoteza fainali ya pili mtawalia katika michuano ya Euro

Aidha mwaka 2018 timu hiyo pia ilitupwa nje ya michuano ya kombe la Dunia hatua ya nusu fainali

Ni takribani sasa miaka 58 Uingereza haijashinda taji la mashindano yoyote

Shirikisho la Mpira wa Miguu Uingereza FA limesema mchakato wa kumteua mrithi wake unaendelea


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.