Jobe apewa Thank You Simba

Joel JJ By Joel JJ β€’ 16th July 2024


Jobe apewa Thank You Simba

Klabu ya Simba imetangaza kuachana na mshambuliaji Pa Omary Jobe ikiwa miezi sita tu tangu alipojiunga na Wekundu hao wa Msimbazi

Taarifa iliyotolewa na Simba mapema leo, imebainisha kuwa uamuzi huo umefikiwa baada ya nakubaliana ya pande mbili

Katika kipindi alichoitumikia Simba, Jobe alishindwa kuonyesha makali yake akifunga bao moja pekee

Lilikuwa ni suala la muda tu Jobe kupewa mkono wa kwaheri kwani aliachwa jijini Dar es salaam wakati wachezaji wengine wakisafiri Misri kwa ajili ya pre-season


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.