Baada ya Hamisa Mobetto kuhusishwa na nyota wa Yanga, Stephane Azizi Ki, mwanamitindo huyo amevunja ukimya juu ya sakata hilo
Hamisa amesema picha na video zinazoendelea katika mitandao ya kijamii kati yake na Ki ni kwa sababu ni rafiki yake wa karibu
"Nilimwambia Azizi Ki asiondoke, ndio mana niliandika maneno kama angeondoka ingekuwaje? Na kama Azizi Ki angeondoka ningepanda ndege kumfata popote alipo, "alisema Hamisa na kuongeza kuwa Ki ni mchezaji mzuri
“Binafsi sikufatwa na mtu yoyote kumshawishi Azizi Ki kubaki, bali nilimshauri tu na yeye ameamua mwenyewe ukizingatia ni mchezaji mzuri anastahili kuendelea kucheza Yanga"


Aziz Ki amesaini mkataba wa miaka miwili kuendelea kuitumikia Yanga ambao utamuweka mikononi mwa Wananchi hadi mwaka 2026



