Klabu ya Azam Fc imefanikiwa kuinasa saini ya kiungo mshambuliaji wa Kimataifa wa Mali, Cheickna Diakite, kutoka klau ya Real Bamako
Nyota huyo chipukizi, 19, aliyepachikwa jina la staa wa Real Madrid Mbappe, kutokana na kasi na uwezo wake wa kuipenya safu ya ulinzi ya timu pinzani, amesaini mkataba wa miaka mitatu utakaomfanya kudumu ndani viunga vya Azam Complex hadi mwaka 2027
Diakite ametua Azam Fc kuchukua nafasi ya Kipre Junior ambaye ametimkia klabu ya MC Algiers
Azam Fc tayari wamethibitisha usajili wa winga huyo ambaye amewahi kuhusishwa na vigogo wa soka nchini klabu za Yanga na Simba



