Klabu ya Yanga imepokea hukumu ya kutotambulika kwa Baraza la Wadhamini la klabu hiyo kufuatia hukumu iliyotolewa Agosti 2, 2023 na Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu
Hukumu hiyo inatokana na kesi ya msingi iliyofunguliwa Agosti 4,2022 na walalamikaji Juma Ally na Geoffrey Mwaipopo, wakitaka kutotambulika kwa Baraza la wadhamini la Yanga lililowekwa madarakani kwa katiba ya mwaka 2010, kukosa sifa kisheria
Aidha, walalamikaji pia walitaka miamala yote ya fedha iliyoidhinishwa na baraza hilo, kutotambulika kisheria kwa kuwa ni batili
Hukumu hiyo, imeitaka bodi iliyokuwa madarakani kwa katiba ya mwaka 1968 iliyofanyiwa mabadiliko mwaka 2011, kurudi madarakani kuongoza klabu ya Yanga
Baraza linalolamikiwa linaongozwa na Mwenyekiti George Mkuchika na wajumbe wake Mama Fatma Karume, Dk Mwigulu Nchemba, Tarimba Abbas na Antony Mavunde.
Mwanaspoti



