Manara amaliza adhabu ya TFF

Joel JJ By Joel JJ β€’ 22nd July 2024


Manara amaliza adhabu ya TFF

Aliyekuwa Msemaji wa Yanga Haji Manara amemaliza kifungo chake cha miaka miwili kilichohusu masuala ya soka

Leo Manara alikwenda kulipa faini ya Tsh Milioni 10 kwa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) na hivyo rasmi sasa yuko huru kuendelea na majukumu yake kama mdau wa soka nchini

Akizungumza na waandishi wa Habari mapema leo, Manara alisema yeye bado ni mwajiriwa wa klabu ya Yanga mpaka 2026 hivyo anaisubiri klabu irejee nchini kufahamu kama anaendelea na majukumu yake ya awali au atapangiwa majukumu mapya

Manara amemshukuru Mdhamini/Mfadhili wa Yanga Ghalib Said Mohammed 'GSM' kwa kumlipa mshahara kwa kipindi chote alichokuwa amefungiwa

Aidha Manara amesema mwaka uliopita aliongezewa mkataba ikiwa ni pamoja na kupandishwa mshahara ambapo ataendelea kuwa mwanafamilia wa Yanga mpaka 2026

"Juzi niliwatuma watu wangu kwenda TFF kwa bahati mbaya hawakufanikiwa ila leo asubuhi na mapema walienda tena na risiti za Benki yenye hundi ya Milioni 10 . Tayari nimeshalipa fedha asante kwa wote waliofanikisha hili naomba tuungane ili tuuendeleze mpira wetu"

"Nakumbuka siku ya mwisho nilifungiwa kama Msemaji wa klabu yangu pendwa ya Yanga tayari adhabu yangu imeisha kwasasa nausubiri uongozi urejee nchini. Wote mtafahamu ni majukumu gani nitapangiwa na uongozi baada ya adhabu yangu," alisema Manara


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.