Sasa ni suala la muda klabu ya Yanga itamaliza sintofahamu kuhusu usajili wa mshambuliaji Jean Baleke ambaye ametua kwa Wananchi kwa mkopo wa msimu mzima
Wakati juzi Baleke anaitumikia na kuifungia Yanga bao katika mchezo dhidi ya Ausburg, mabosi wa Yanga na Mazembe walikuwa wakikamilisha taratibu za nyota huyo kujiunga na Yanga akiwa ametoka kuitumikia Al Ittihad ya Tripoli, Libya
Kupitia taarifa rasmi iliyotolewa na TP Mazembe katika tovuti yao, wameidhinisha Baleke kuitumikia Yanga kwa mkopo wa msimu mzima
"Miezi sita baada ya kuondoka Tanzania, Jean Othos BALEKE atarejea huko, akiwa na rangi tofauti. Mshambulizi huyo mwenye umri wa miaka 23, ambaye bado ana mkataba na TP Mazembe, ametolewa kwa mkopo tena lakini kwa Young Africans"
"Baada ya msimu mmoja na nusu kukaa Simba SC, BALEKE alienda kwa mkopo Libya, Al Ittihad ya Tripoli. Uongozi wa TPM ulikubali masharti ya mkopo wa mchezaji huyo kwa ajili ya Young Africans," ilibainisha taarifa ya TPM
Licha ya kuonekana viunga vya Avic Town tangu mwanzoni mwa mwezi huu, Yanga haikuwa imemtambulisha rasmi Baleke kwa kuwa ilikuwa katika mchakato wa kukamilisha usajili
Ni wazi sasa wananchi wameunasa mtambo huo wa mabao, August 08 atakuwepo uwanja wa Benjamin Mkapa!



