Mchezo wa pili wa Mpumalanga Premier's International Cup kati ya TS Galaxy dhidi ya Yanga, utakaopigwa Jumatano, Julai 24, utaonyeshwa mbashara na vituo vya televisheni
Awali ilitangazwa mchezo huo usingeonyeshwa wala mashabiki kuruhusiwa kuingia uwanjani
Lakini hatimaye timu husika na waandaaji wa michuano hiyo wameridhia mechi hiyo irushwe mbashara
Azam TV wamethibitisha, watakuwa live kurusha mchezo huo




