Simba yapania usajili wa Mpanzu

Joel JJ By Joel JJ β€’ 27th July 2024


Simba yapania usajili wa Mpanzu

Mabosi wa Simba wamelazimika kufungua tena mazungumzo kumsajili kiungo mshambuliaji wa AS Vita Elie Mpanzu ambaye unaweza kusema katika dirisha hili la usajili ndiye mchezaji ambaye tetesi za usajili wake zimezungumzwa kwa muda mrefu zaidi

Baada ya sintofahamu ya Kibu Denis aliyetorokea Ulaya, ni wazi Simba inalazimika kusajili mchezaji wa kuziba nafasi yake

Ili kupata mchezaji wa daraja la juu, Simba inalazimika kuangalia tena nje ya nchi uamuzi ambao pia utawalazimu kuachana na mchezaji mmoja zaidi wa kigeni

Jana tetesi za Simba kurejea tena kwa Mpanzu zikaanza kuvuma ambapo taarifa zilibainisha kuwa Simba iliongeza dau ili kuishawishi AS Vita kumuachia winga huyo ambaye kwa sasa ndiye mchezaji bora wa Vita

Wadadisi wa masuala ya usajili wanasema kuna nafasi kubwa Simba itafanikiwa kumsajili winga huyo ambaye tayari alishafikia makubaliano binafsi juu ya maslahi yake pale atakapojiunga na Simba

Pengine Mpanzu alipaswa kuwa mchezaji wa kwanza kusajiliwa na Simba katika dirisha hili lakini ilitokea sintofahamu kuhusu mkataba wake

Mwenyewe alisema amemaliza mkataba na AS Vita lakini klabu hiyo ikakanusha na kuthibitisha kuwa Mpanzu bado ana mkataba wa mwaka mmoja

Changamoto ikawa dau ambalo Vita wanataka ambapo Mnyama atalazimika kutoa zaidi ya Milioni 600 kununua mkataba wake wa mwaka mmoja uliobaki

Wakati huu Simba imerejea ikiwa 'serious' na pengine ile kiu ya Wanamsimbazi kumuona Mpanzu akivaa uzi wa Mnyama inaweza kufanikiwa


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.