Kaizer Chiefs, Yanga kuchuana Jumapili

Joel JJ By Joel JJ β€’ 27th July 2024


Kaizer Chiefs, Yanga kuchuana Jumapili

Kocha Mkuu wa Yanga Miguel Gamondi amesema anatarajia mchezo wa Toyota Cup dhidi ya Kaizer Chiefs utakaopigwa Jumapili, utakuwa maandalizi mazuri kwa kila timu kuelekea msimu mpya wa mashindano

Akizungumza katika Mkutano na waandishi wa habari ambao ulihusisha makocha wa timu zote, Gamondi alisema mchezo utakuwa na ushindani akiamini Kaizer Chiefs watakuja na ari kubwa kufuatia ujio wa Kocha Nasreddine Nabi

"Mchezo wetu dhidi ya Kaizer Chiefs utakuwa mchezo mzuri na wenye ushindani hasa ukizingatia Chiefs wana Mwalimu mpya na kila mchezaji atapata nafasi ya kumuonyesha Mwalimu uwezo wake na kwetu sisi pia maandalizi yetu yanazidi kuimarika na tunaamini tutakwenda kuwa na mechi nzuri," alisema Gamondi

Aidha Kocha huyo raia wa Argentina amesema maandalizi ambayo Yanga wamepata hapo Afrika Kusini ni faida kubwa kwao lakini pia wameweza kuitangaza Yanga Kimataifa

"Yanga ujio wetu hapa Afrika Kusini umekuwa muhimu sana kwetu kwenye maandalizi kuelekea msimu mpya wa 2024/25 na kucheza na timu inayoshiriki Ligi Kuu ya Ujerumani (Bundesliga) ni sehemu ya kuendelea kuitangaza Klabu yetu barani Afrika na Duniani kote," alisema

Yanga ilitua Johanesurg jana tayari kwa mchezo huo utakaopigwa Jumapili katika uwanja wa Toyota


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.