Yanga, Azam Fc kuchuana fainali Ngao ya Jamii

Joel JJ By Joel JJ β€’ 8th August 2024


Yanga, Azam Fc kuchuana fainali Ngao ya Jamii

Yanga na Azam Fc zitacheza fainali ya Ngao ya Jamii baada ya kushinda mechi za nusu fainali leo

Mchezo uliomalizika usiku huu, Yanga imeendeleza ubabe dhidi ya watani zao Simba baada ya ushindi wa bao 1-0 katika mchezo uliopigwa uwanja wa Benjamin Mkapa

Bao pekee la Yanga lilifungwa na Maxi Nzengeli katika dakika ya 44 ya mchezo

Ulikuwa mchezo wenye upinzani mkali lakini ni wazi Yanga imeendelea kuibuka kidedea dhidi ya watani zao ukiwa mchezo wa tatu mfululizo wanashinda

Mapema Azam Fc ilitinga fainali kibabe kwa kuichapa Coastal Union mabao 5-2 katika mchezo uliopigwa uwanja wa New Amaan Complex visiwani Zanzibar

Yanga na Azam Fc sasa zitakutana kwenye fainali ya Ngao ya Jamii August 11 wakati Simba ikichuana na Coastal Union kusaka nafasi ya tatu


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.