Yanga na Azam Fc zitacheza fainali ya Ngao ya Jamii baada ya kushinda mechi za nusu fainali leo
Mchezo uliomalizika usiku huu, Yanga imeendeleza ubabe dhidi ya watani zao Simba baada ya ushindi wa bao 1-0 katika mchezo uliopigwa uwanja wa Benjamin Mkapa
Bao pekee la Yanga lilifungwa na Maxi Nzengeli katika dakika ya 44 ya mchezo
Ulikuwa mchezo wenye upinzani mkali lakini ni wazi Yanga imeendelea kuibuka kidedea dhidi ya watani zao ukiwa mchezo wa tatu mfululizo wanashinda
Mapema Azam Fc ilitinga fainali kibabe kwa kuichapa Coastal Union mabao 5-2 katika mchezo uliopigwa uwanja wa New Amaan Complex visiwani Zanzibar
Yanga na Azam Fc sasa zitakutana kwenye fainali ya Ngao ya Jamii August 11 wakati Simba ikichuana na Coastal Union kusaka nafasi ya tatu



