Simba Queens imeanza vyema michuano ya CECAFA kuwania ubingwa wa ukanda wa Afrika Mashariki kwa soka la Wanawake wakiifumua Fad Djibouti mabao 5-0
Mchezo huo ulichelewa kuanza baada ya mvua kubwa zinazoendelea kunyesha Ethiopia kujaza maji uwanja
Hata hivyo changamoto hiyo haikuvuruga mipango ya Kocha Juma Mgunda ambaye amepania kutwaa taji hilo ili kuipa Simba Queens tiketi ya kushiriki michuano ya Ligi ya Mabingwa ya Wanawake msimu huu
Mabao ya Simba Queens yalifungwa na Jentrix Shikangwa, Elizabeth Wambui huku Aisha Rashid akifunga mabao matatu 'hat-trik'




